FALSAFA , HISTORIA YA CHAMA CHA
WATAFUTA NJIA.
Chama
cha Watafuta Njia ni Kanisa lililojikita zaidi katika mambo ya Kiroho pia huwa
na programu za Maburudisho kwa Vijana wa
Umri wa Miaka 10 -15.
Ni
mipango na malengo ya Kanisa la Waadventista Wasabato ,linawajibika
kuwatengenezea programu zinazowiana na zitakazowavutia Vijana kwa kufanya
yafuatayo:
(i)
Kuwafundisha kwamba Mungu huwapenda na
hujali katika maisha yao yote.
(ii)
Kuwatia moyo Watafuta Njia kugundua kwamba uwezo walionao wamepewa na Mungu na
ndiye mtoaji wa vipawa.
(iii)
Kuwatia moyo vijana kwamba wao wanapendwa na
Mungu.
(iv)
Kutambua kwamba wokovu ni kwa mtu na ndilo
hitaji la Chama.
(v)
Kumjengea Mtafuta Njia kuishi kiafya na
kufurahia Uumbaji wa Mungu.
(vi)
Kumfundisha Mtafuta Njia njia ifaayo na
mambo yatakayomridhisha na kufaulu
katika maisha yake ya sasa na baadaye.
(vii)
Kuwatia moyo Watafuta Njia kutunza afya zao.
(viii)
Kuwapa nafasi na kuwaandaa katika Uongozi.
(ix)
Kuomba kwa ajili ya kutunza afya zao pamoja
na maendeleo ya Kijamii , kiakili na maisha ya kila Mtafuta Njia.
HISTORIA
YA CHAMA CHA WATAFUTANJIA.
Kuanzia 1900 – 1907
baadhi ya Makanisa walianzisha Ushirika wa Vijana Wadogo
Mwanzoni mwa 1930
liliingia wazo la kuwa na “ PATHFINDER” katika Calfonia ya Kusini
Mashariki , mwaka uliofuata walifanya
Kambi la kwanza huko Bernadin Mountains. Eneo hilo lilinunuliwa kwa ajili ya
kufanyia makambi kwa ajili ya shughuli za Vijana likiwa na ukubwa wa ekari 15 na kuitwa “Junior Missionary Camp”
Mwaka 1930 John Mckim
Kiongozi wa Scout aliamua kuanzisha Kikundi cha Vijana Wadogo wa Kanisa la St.
Anna . Aliamini kwamba kama Kanisa linahitaji kuwa na kikundi kwa ajili ya
mambo ya Kiroho zaidi badala ya shughuliza za Scout. Dr. Theron Johnson alitoa
nyumba yake kama sehemu ya kukutania. Nyumba hiyo ipo mpaka leo. Walikutana
chini na Wasichana walikutana juu ghorofani na Mrs. Claude Stein alichaguliwa
kuwa Mkurugenzi wa Wasichana na Mume wake walikuwa Washiriki wa Kanisa la
Waadaventista Wasabato Fulleston waliamua
kutumia” JINA PATHFINDER”
Mwanzoni mambo
yalikwenda vizuri ,lakini baadaye yalibadilika, upinzani ulianza washiriki
wengi Kanisa walifikiri kwamba Vijana hawa wanajifunza mambo yasiyoendana na
Maadili ya Kiadventista. Shughuli nyingi zilizofanyika wakati ule ni zile
zinazofanyika leo na Vijana wetu, kama Michezo, Ukambikaji,na Masomo ya Viumbe
vya Asili, Safari za Nje, n.k, lakini muda ulikuwa haujafika kwa Kanisa la St.
Anna kuwa na kikundi cha Watafuta Njia.
Baraza la Kanisa
lilimtaka Mzee Mckim na Johnson wavunje kikundi hicho mara
moja vinginevyo hatua za kinidhamu
zitachukuliwa dhidi yao, huduma za Watafuta Njia zilikoma , hadi Vita Kuu ya
Pili ya Dunia.
Mwaka 1930 na 1940 Bwana Lawrence Skiner aliamusha wazo la kuwa na
Chama cha Watafuta Njia baada ya kuitwa kufanya kazi Kusini Mashariki mwa
Calfonia kuwa Mkurugenzi wa Vijana
Wadogo Makanisani, lakini alishauriwa na Jenero Konferensi kuendeleza Jina la
JMV badala ya kuanzisha Jina Jipya kama Watafuta Njia. Mwaka 1946 John. H.
Harmrock alibuni Nembo yenye sura ya
Pembe Tatu iliyosimamia mambo ya Kiroho ,Kimwili, na Kijamii kulingana na
maendeleo ya Mtoto . Utatu Mtakatifu:
Mungu
Baba
Mungu
Mwana na,
Roho
Mtakatifu.
Baadaye Vyama vya Watafuta Njia vilianzishwa katika sehemu za River
Side na Glendale vilianzishwa 1946 na 1947 kasi ya uanzishwaji iliongezeka
zaidi Mzee Skiner Mkurugenzi wa Vijana
wa Jenero Konferensi aliamini kwamba wakati ulikuwa umefika wa kuanzisha Chama
hiki cha pekee na mwaka 1947 -1950 Jina Jipya la Vijana Wadogo toka JMV na kuwa
Pathfinder lilifanikiwa zaidi. Mwaka 1950 CHAMA CHA WATAFUTA NJIA kilianzishwa
rasmi “Pathfinder lilipitishwa badala ya JMV. Mwaka 1949 --- - - Wakurugenzi wa
Vijana walimpendekeza Henry Bergh atayarishe Wimbo wa Watafuta Njia na mwaka huo huo Wimbo huo ulikuwa tayari:
Tuwatafuta
njia shujaa
Watumishi
wa Mungu na
Tu
waaminifu wa Kweli
Na Safi, pia tunao Ujumbe
Unaotukomboa,
Yesu Mfalme
Arudi
tena kwako nami.
Mwaka 1948 Bwana Henry Bergh alibuni Bendera ya Watafuta Njia na mwaka
huo huo Mama Helen Hobbs alishona Bendera ya Kwanza ya Watafuta Njia Lawrence
Paulson wa Glendale alibuni na kufaulu kutoa kwa mfululizo Vitabu kwa ajili ya Vilabu vya Watafuta Njia pamoja na Shule za Kanisa hii ikijumuisha
Mahitaji ya Madarasa ya Vijana. Mwaka 1962
Bwana Clark Smith na Henry Garlick walitunga Mwongozo wa Kwata ( Drill
Manuals)
Mwaka 1950 Lawrence Skiner na John Honcock walikutana Washington kwa
ajili ya kutayarisha Mwongozo kwa ajili ya Viongozi wa Watafuta Njia na Mwongozo wa namna ya Kuanzisha Chama cha Watafuta Njia. Programu na Nembo
vilikubaliwa Kiulimwengu lakini
walitumia Lugha tofauti tofauti kutokana
na utafisiri.
Nchi zilizoongea
Kihisipania walitumia Conquistadors
Nchi za Kireno “
Desbravadors”
Nchi za
Kifaransa walitumia jina la “Enlair”
Programu za Watafuta Njia ziliendelea Maonesho ya Kwanza yalifanyika
huko Dinuba, Calfonia Septemba 23,1951.Mwaka 1954 Kamporii ya Kwanza ilifanyika
Ulimwenguni. Vyama vya Watafuta Njia vilihudumia wale ambao hawajapevuka , na
mwaka 1962 Mkurugenzi wa Vijana wa Kaskazini aliboresha programu ya Watafuta
Njia waliopevuka alitumia chama cha Chuo cha Pacific Union kama kielelezo ,
1964 Programu ya Watafuta Njia
Waliopevuka ya Konferensi ya Calfonia Kusini Mashariki iliimarishwa.
UONGOZI WA WATAFUTA NJIA NGAZI YA JENERO KONFERENSI.
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
||||||||||||
|
KUWAELEWA
WATAFUTA NJIA.
Ulinganifu wa pekee
unahitajika kwa ajili ya kuwaelewa na kutambua tofauti za Mahitaji yao ambayo hudhihirisha katika
ukuaji wao kufuatana na vipindi vifuatavyo:
= Pre –
Adolesence 9 - 12
= Ealy
Adolesence 13 – 15
PRE – ADOLESENCE.
Umri wa Vijana huanzia miaka 9
-12 ni Vijana walio na makelele mengi hawatulii, hawako makini katika kazi zao,
ukuaji wao ni wa taratibu sana ,pia huwa
na afya njema , lakini wasichana hukua kwa haraka zaidi kuliko wavulana pia watu wenye jaziba katika mambo yao mengi.
Baada ya miaka 12 huanza kukua kwa haraka na kuanza kurefuka hata miili yao
huanza kurefuka hadi kufikia miaka 17 -18. Hiki ni kipindi cha ukuaji huanza
kujitegemea kimawazo.
TABIA ZAO KIAKILI;
(i)
Vijana wa
umri huu hutunza kumbukumbu kama sumaku kwa ajili ya kupokea mambo mapya,
Hujifunza kwa haraka na hutunza kile walichojifunza.
(ii)
Ni Vijana
wenye bidii na wachunguzi wa mambo na
kujifunza kwayo, hupenda kushika vitu na kujifunza vimetengenezwaje pia hupenda
mambo mapya.
(iii)
Wanapenda
Masimulizi mapya na wachunguzi wa Vitabu
mbalimbali na kuangalia yaliyomo ndani.
(iv)
Hupenda
kukusanya mambo mapya na kuyachunguza. Wataalam wanasema kwamba 90% ya umri huu
wa Watoto hujikusanya wanne,watano hujikusanya kulingana na vivutio mahalia
,hiki ni kpindi kizuri cha kuwafundisha Nishani.
(v)
Hiki sio
kipindi cha kuchagua mambo maalum bali ni kipindi cha kuwaingiza katika Chama
cha Watafuta Njia ,ni kipindi cha uwazi , pia kuwafundisha mambo mapya
pamoja na kutembelea sehemu mbalimbali
,kama vile miezi mitatu kwa ajili ya programu na mwezi mmoja kwa ajili ya
Ufundi Stadi.(matembezi kutembelea sehemu mbalimbali)
TABIA ZA KIMWILI;
(i)
Wana afya njema.
(ii)
Wana uwiano mzuri wa mawasiliano na akili
kama vile michezo,kutembea kwa mwendo mrefu na mambo mbalimbali wanayojifunza.
(iii)
Umri huu
hawawezi kukaa pamoja wakatulia ni muda wa michezo mingi , umri huu ni
wa mazoezi mengi mwalimu vyema achague chumba kwa ajili ya kufanya mazoezi kwa
ajili ya mapafu, pia wanatakiwa kuwa na shughuli nyingi iwezekanavyo.
(iv)
Hupenda kuiga mambo ya makundi na hutegemea
msimamo wa Wazazi kadri wanavyohusiana na Mungu wao.
MAHUSIANO KIJAMII.
(i)
Hependa sana kusifiwa na hutunza siri pamoja na vituko vingi.
(ii)
Hujifunza kwa ushirikiano (kama timu) lakini
wana msimamo wa pekee na hulinda imani yake.
(iii)
Ni watukutu sana na huzurura ovyo na
wachunguzi na wapelelezi wa mambo na wepesi kuiga tabia za watu ,huiga tabia ya
mwalimu ,wazazi.
(iv)
Umri huu
ni wepesi kuamini mwalimu kuliko wazazi wake na hawapendi
kuchanganyikana na jinsia nyingine.
(v)
Wavulana hukaa peke yao na Wasichana peke
yao.
TABIA
ZA KIROHO.
(i)
Hupenda sana mambo ya Kiroho na kufanya kazi
za Kanisa.
(ii)
Ni wakati ufaao na umri mzuri kwa ajili ya
Ubatizo hufanya maamzi thabiti kwa kumtafuta Mungu.
(iii)
Umri huu pia ni mashahidi waaminifu na
hubiri Injili kwa njia ya matendo yao na maisha yao na hujiweka wakfu kwa
Mungu.
(iv)
Ni wepesi kuamini hivyo ni vema pia ni
rahisi kufundisha Dini.
VIJANA WA UMRI WA MIAKA 13 – 15.
( EARLY ADOLESENCE)
Kipindi hiki ukuaji wake ni wa haraka pi ni wavivu katika kufanya kazi
kwasababu ya uwiano wa akili na mwili, mfadhaiko kwa Vijana wa umri huu
husababishwa na baadhi ya viungo kama vile pua , mdomo,na miguu hukua kwa
haraka kuliko viungo vingine vya mwili.
Huwafanya wajisikie vibaya husababisha wajione si wa muhimu , pia urefu
huanza kupungua na hukoma, badala yake hupenda kuchanganyika na jinsia tofauti
wasichana kwa wavulana, na mapenzi ya
ngono huanza.
Kutokana na maendeleo ya akili huweka bayana na husababisha Vijana wa
umri huu huanza kuangalia mambo binafsi kuliko kuamini Neno la Mungu kuliko
kipindi
kilichopita. Wakati wote ni kipindi hiki ni cha ndoto na huanza
kufikiria mambo yajayo kwamba atafanya nini badaye.
Vijana hawa hupenda mambo yanayowapendeza na huwaangalifu nayo ili
yasiharibike au mipango yao isiharibike.Changamoto walizo nazo ni kupenda mambo
ya starehe ambayo huchukua nafasi ya
mapenzi ya mambo ya Kiroho na huona jambo tu la kawaida katika mambo ya Mungu.
TABIA ZA KIAKILI.
(i)
Ni waangalifu sana na somo kuu katika
kipindi hiki , wana ndoto juu ya maisha yajayo kwamba atafanya nini.
(ii)
Hujifunza kwa haraka mambo mapya.
(iii)
Wavulana alimia kubwa hupenda masomo ya
Sayansi na masomo mbalimbali na Wasichana hupenda zaidi mabo ya nyumbani.
(iv)
Anahitaji kutambuliwa kwamba anamchango
mkubwa katika jamii.
(v)
Huyakubali matendo yake.
TABIA ZA KIMWILI.
(i)
wana afya njema mwili wao huvutia.
(ii)
Mwili wao hukua kwa haraka zaidi na huanza kupenda aina ya vyakula fulani.
(iii)
Mifupa ya mwili hutanuka ,pia hupoteza
mawasiliano kwasababu ya uwiano wa mwili kwasababu umbile alilo nalo na mshipa
mkuu hukua kwa haraka.
(iv)
Via vya Uzazi hukua ,mabadiliko ya kukua hutokea;
Homoni mpya ambayo hukuza via vya Uzazi huathiri tabia ya mhusika
kutokana na mabadiliko hayo. Bwana
Rousseau kwamba:
tunazaliwa
mara mbili , mara ya kwanza huzaliwa kutok
a kwa
Mama. Na mara ya pili huzaliwa katika maisha am
bacho huwa
mshirika.
(v)
Wasichana kwa kawaida ni warefu kuliko
wavulana wa miaka 12 na 13 ,miaka 14 ni
wembamba na warefu pia miaka 15 na miaka 15 ni miaka 15 vijana wa umri
ni wafupi hutofautiana kwa inchi 2 na Vijana wa miaka 16 na wengine hawana
tofauti sana na wengine.
TABIA ZA KIJAMII.
-Vijana wa umri huu ni waaminifu kwa rika yao ,miongoni mwao ni wacha
Mungu.
Hupenda kusifiwa na kutambuliwa na makundi mengine katika shughuli
wazifanyazo, Hupendwa kuungwa mkono na
jamii. Uchaguzi wa mambo muhimu huanza katika umri huu.Jambo la pekee katika ni
kuwafundisha namna ya kujitambua kabla ya kufikia kwamba ni kipindi cha hatari
maishani mwao. Ni vema wafundishwe kazi ya utumishi kwa ajili ya kazi ya Mungu. Mara nyingi huwa
na ukinzani na wasiwasi juu ya maisha yao.